Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Tamima Haji Abass
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. TAMIMA HAJI ABASS aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kutoa elimu kuhusu uwepo wa Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF) ili wanawake wengi zaidi wanufaike na mikopo?
Supplementary Question 1
MHE. TAMIMA HAJI ABASS: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni kwa kiasi gani mfuko huu umewanufaisha wanawake tangu umeanzishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali ina mkakati gani wa kusimamia marejesho kwa wakopaji wa mfuko huu?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Tamima kwa maswali mazuri. Hadi sasa sisi kama Wizara ni zaidi ya shilingi 1,400,000,000, tayari wanawake wameweza kunufaika na masharti ni nafuu. Kuhusu kusimamia marejesho, hii ni kazi yetu sisi sote viongozi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaendelea kutoa elimu kwa wenzetu ambao tunawasemea, na vilevile kabla ya kupewa fedha wanapewa elimu ya fedha, lipa kwa hekima na vilevile rejesha kwa wakati. Kwa hiyo, tunaendelea kuona kwamba wapewe ndani ya mfuko ukiwa ndani ya Wizara kwa masharti nafuu, kabla hawajaendelea na usumbufu wa marejesho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukapeleka hili kwenye vyombo vyetu vya fedha, kule ambako mpaka sasa wengi wetu tumeona kwamba wanalalamika masharti ni mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, sisi kwa umoja wetu Waheshimiwa Wabunge, kila mmoja ana kundi kubwa nyuma yake, kila mmoja akiweza kusisitiza mtu akope na kulipa kwa wakati, basi wengi wataweza kurejesha ili wengi waweze kukopa.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved