Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 1 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Stella Simon Fiyao
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Mlowo – Isansa – Magamba hadi Mkwajuni Wilaya ya Songwe?
					
 
									Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwa ajili ya kuiboresha Barabara ya Mlowo – Isansa – Magamba hadi Mkwajuni ambapo katika mwaka 2019/2020, Serikali ilipeleka shilingi 294,630,000.00 kwa ajili ya kufungua barabara hii kipande chenye urefu wa kilomita 16.2 eneo la Magamba hadi Ilumbwe. Aidha, katika mwaka 2022/2023, Serikali ilitumia shilingi 75,684,400.00 kujenga Solid Drift safu mbili, box kalavati kubwa moja (two cells) na mifereji ya maji ya mvua mita 70. 
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika mwaka wa fedha 2022/2023 na 2023/2024, Serikali imetumia shilingi 365,395,000.00 kufanya matengenezo ya barabara kipande chenye urefu wa kilomita 13.1 kuanzia Mlowo hadi Isansa ambazo zimefanya kazi ya kuumba tuta la barabara kilometa 13.1, kuweka changarawe na kushindilia, kujenga safu saba za kalavati pamoja na kujenga mifereji ya maji ya mvua yenye urefu wa mita 1085.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuiboresha barabara hii kwa kuijenga na kuifanyia matengenezo mara kwa mara ili kuiimarisha zaidi kulingana na upatikanaji wa fedha.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved