Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 2 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Amb. Liberata Rutageruka Mulamula
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Nominated
Primary Question
						MHE. BALOZI LIBERATA R. MULAMULA aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Zahanati Kitongoji cha Kakoni - Misenyi ili iweze kuhudumia wananchi wa Kitongoji hicho na jirani?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- 
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea na ujenzi wa zahanati katika vijiji na mitaa inayokidhi vigezo ili kusogeza huduma za afya ya msingi karibu na wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2020/2021 hadi 2024/2025, Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi imepelekewa jumla ya shilingi milioni 400 kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati nane. 
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na mwongozo wa Serikali wa Ujenzi wa Vituo vya kutolea Huduma za Afya ngazi ya msingi unaelekeza ujenzi wa zahanati kwenye ngazi ya kijiji. Aidha, Kakoni ni miongoni mwa Kitongoji katika Kijiji cha Kitobo ambacho tayari kina zahanati. Hivyo, kwa mujibu wa mwongozo, Kitongoji cha Kakoni kitahudumiwa na Zahanati ya Kitobo.  Ahsante.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved