Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 4 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Vita Rashid Kawawa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Primary Question
						MHE.  VITA R. KAWAWA aliuliza:-
Je, lini Serikali itavipatia Magari ya kubebea wagonjwa Vituo vya Afya vya Magazini na Lusewa – Namtumbo?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 ilinunua magari 594 ya kubebea wagonjwa na usimamizi wa huduma za afya katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. 
Mheshimiwa Naibu Spika, magari haya yamesambazwa kwenye Halmashauri kwa wastani wa magari mawili hadi manne kwa kila Halmashauri, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo imepokea magari mawili ya kubebea wagonjwa. Magari hayo yanatumika katika Hospitali ya Wilaya ya Namtumbo na Kituo cha Afya cha Mtakanini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutekeleza mipango ya kununua magari ya kubebea wagonjwa kwa ajili ya vituo vya afya nchini vikiwemo Vituo vya Afya vya Magazini na Lusewa – Namtumbo.  Ahsante.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved