Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 5 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Joseph Anania Tadayo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwanga
Primary Question
						MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa zahanati iliyoboreshwa ya Mangio iliyopo Kata ya Mwaniko, Wilayani Mwanga?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Zahanati ya Mangio ilianzishwa kwa nguvu za wananchi mwaka 2010 na baadaye kuendelea kukamilishwa kupitia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri, Serikali Kuu na Mfuko wa Jimbo ambapo jumla ya shilingi milioni 74 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo, ambapo kwa sasa iko 85% ya ujenzi.  
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga imetenga shilingi milioni 20 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa zahanati ya Mangio.  Ahsante.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved