Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Planning and Investment | Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji | 6 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Saashisha Elinikyo Mafuwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Hai
Primary Question
						MHE.  SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:-
Je serikali ina mpango gani wa njia mbadala ya kukuza uchumi wa wananchi wa Hai kutokana na uhaba wa ardhi ya uzalishaji?
					
 
									Name
Stanslaus Haroon Nyongo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Maswa Mashariki
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali ili kuwawezesha wananchi kukua kiuchumi wakiwemo wananchi wa Wilaya ya Hai. Mikakati hiyo ni pamoja na:-
Kutoa Mikopo yenye riba nafuu hususan kwa wanawake, vijana na walemavu; Kujenga mfumo wa kidijitali vijijini ili kuongeza matumizi ya TEHAMA katika shughuli za kiuchumi; na Kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia uwekezaji, hasa katika Sekta ya Viwanda. 
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Wilaya ya Hai, Serikali imeendelea kuhakikisha Mradi wa Kiwanda cha KMTC (Kilimanjaro Machine Tools Company) ambacho kiko chini ya NDC unatekelezwa. Aidha, Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Hai imetenga eneo maalum la uwekezaji lenye ukubwa wa hekta 463 ambalo linaendelea kutangazwa kwa wawekezaji mbalimbali. Hivyo, Serikali itaendelea kuhimiza na kutangaza fursa zinazopatikana katika Wilaya ya Hai ikiwemo fursa za Utalii ili kuimarisha uchumi wa wananchi.  Ahsante sana. 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved