Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 7 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Muharami Shabani Mkenge
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bagamoyo
Primary Question
						MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:-
Je, lini umeme utapelekwa katika eneo la Kitame, Kata ya Makurunge ili kuwasaidia wazalishaji wa chumvi?
					
 
									Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:- 
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Wilaya ya Bagamoyo, Serikali kupitia REA inaendelea na utekelezaji wa mradi wa kupeleka umeme kwenye maeneo ya migodi midogo yakiwemo maeneo ya wazalishaji wa chumvi kupitia mkandarasi aitwaye Dieynem Company Limited. Hadi kufikia mwezi Machi 2025, jumla ya maeneo 14 ya migodi midogo imepelekewa umeme ambapo kati ya hayo, maeneo matatu ni ya wachimbaji wa chumvi wanaopatikana katika eneo la Kitame Kata ya Makurunge, ambapo jumla ya wachimbaji 34 wanaopatikana katika maeneo hayo wamefikiwa na huduma ya umeme. 
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme kwa wachimbaji wa chumvi waliosalia itaendelea kulingana na upatikanaji wa fedha.  Ahsante.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved