Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 9 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Hassan Zidadu Kungu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduru Kaskazini
Primary Question
						MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Mradi wa Maji Kata ya Matemanga katika Vijiji vya Milonde, Matemanga na Changarawe – Tunduru?
					
 
									Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Vijiji vya Milonde, Matemanga na Changarawe vilivyopo Kata ya Matemanga Wilayani Tunduru vinapata huduma ya majisafi na salama kupitia vyanzo vya maji vya Mkwinda na Namalowe. Mradi huo ulijengwa mwaka 1980 na baadaye kwa nyakati tofauti kufanyiwa ukarabati katika vipindi viwili tofauti vya mwaka 2012 na 2021 ili kuboresha ufanisi katika utoaji wa huduma wa skimu hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto ya ongezeko la mahitaji ya huduma ya maji kwa wananchi wa Kata ya Matemanga kutokana na ongezeko la idadi ya watu ambapo kwa sasa imefikia zaidi ya watu 10,000. Serikali katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, itajenga tanki lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 500,000 ili kuongeza uzalishaji kutoka lita 275,000 za sasa kwa siku na kufikia lita 775,000. Lengo ni kuhakikisha wananchi wa Kata ya Matemanga wanapata huduma ya majisafi, salama na yenye kutosheleza.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved