Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 12 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Issaay Zacharia Paulo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbulu Mjini
Primary Question
						MHE. REGINA N. QWARAY K.n.y. MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza gharama ya matibabu ya kusafisha figo katika hospitali zetu nchini?
					
 
									Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
						NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imechukua hatua mbalimbali ili kupunguza gharama za kusafisha figo, ikiwa ni pamoja na kusogeza huduma hizi kwa kuongeza vituo vya dialysis katika hospitali 15 za rufaa za mikoa, na hospitali zote za kanda nchini. 
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, Serikali itaongeza wadau na taasisi zinazoingiza vitendanishi, vifaatiba na dawa zitumikazo badala ya kuacha mtu mmoja au taasisi kutawala soko bila kuruhusu ushindani na pia kuhamasisha viwanda na ubunifu ndani ya nchi. Aidha, Serikali imesambaza kwenye hospitali za rufaa za mikoa nchini mashine zaidi ya 100 pamoja na vitendanishi vyake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe rai kwa wananchi, mara utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote utakapoanza, waweze kujiunga, kwani ndiyo njia pekee ya kuweza kuwasaidia kuepukana na gharama za matibabu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved