Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 14 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Jacquline Andrew Kainja
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaona haja ya kuwa na kiwanda cha asali Tarafa ya Kiwele – Sikonge?
					
 
									Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
						NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Sikonge ina tarafa mbili ambazo ni Tarafa za Sikonge na Tarafa ya Kiwele. Serikali kupitia Mfuko wa Huduma za Misitu Tanzania (Tanzania Forest Services) ilijenga kiwanda cha kuchakata mazao ya nyuki Tarafa ya Sikonge. Kiwanda hicho kina uwezo wa kuchakata asali tani nne kwa siku. 
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kukidhi mahitaji ya kiwanda kilichojengwa, sasa Serikali itaanza mchakato wa awali wa kujenga kiwanda cha pili cha kuchakata mazao ya nyuki, ikiwa ni pamoja na kuainisha uwezo wa uzalishaji wa asali kwa Tarafa ya Kiwele. Ahsante.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved