Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 1 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 15 | 2025-04-08 | 
 
									Name
Dr. Paulina Daniel Nahato
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza uhaba wa mabweni katika vyuo vikuu vya umma?
					
 
									Name
Prof. Adolf Faustine Mkenda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Rombo
Answer
						WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto ya uhaba wa malazi ya wanafunzi katika vyuo vikuu vya umma nchini. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali inaendelea na ujenzi wa mabweni mapya 26 katika kampasi 12 za vyuo vikuu vya umma nchini. Mabweni haya yakikamilika yatakuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi 5,987 kwa wakati mmoja. Ujenzi wa majengo ya mabweni hayo unatarajiwa kukamilika mwaka 2026.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali inatoa wito kwa sekta binafsi kuwekeza kwenye ujenzi wa hostel katika maeneo ya vyuo vikuu ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma ya malazi kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved