Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 54 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 691 | 2025-06-26 | 
 
									Name
Joseph George Kakunda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sikonge
Primary Question
						MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: -
Je, lini Zahanati za Molemlimani, Muungano, Urafiki, Isanjandugu, Iyombakuzova na Kapumpa zitakamilika?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kujenga vituo vya kutolea huduma na kuvisajili ili vianze kutoa huduma za afya. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2024/2025 jumla ya zahanati 1,158 zimejengwa na kusajiliwa na zinatoa huduma.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2026/2027 Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge itatenga shilingi milioni 250 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya Zahanati za Muungano, Urafiki, Isanjandugu, Iyombakuzova, Kapumpa na Molemlimani. Ahsante. (Makofi) 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved