Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 27 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 341 | 2025-05-19 | 
 
									Name
Rehema Juma Migilla
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Ulyankulu
Primary Question
						MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga sekondari nyingine katika Kata ya Kanindo kwa kuwa Shule ya Sekondari Kanindo ina wanafunzi wengi?
					
 
									Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Shule ya Sekondari Kanindo ina wanafunzi 648 wa kidato cha kwanza hadi kidato cha nne wakijumuisha wavulana 255 na wasichana 393. 
Mheshimiwa Spika, shule hiyo ina vyumba vya madarasa 19 ambavyo vinatosheleza mahitaji kwa wanafunzi waliopo. Aidha, shule ina hosteli inayohudumia wanafunzi wanaotoka maeneo ya mbali kikiwemo Kijiji cha Mbeta. Vilevile, baadhi ya wanafunzi wamehamishiwa shule mpya ya Ikonongo kwa lengo la kuwapunguzia mwendo mrefu wa kutembea.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved