Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 27 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 346 | 2025-05-19 | 
 
									Name
Tamima Haji Abass
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. TAMIMA HAJI ABASS aliuliza:-
 Je, upi mpango wa Serikali kuimarisha mawasiliano ya simu kwenye vijiji vyenye changamoto ya huduma hiyo Mkoa wa Kaskazini Unguja?
					
 
									Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 ilitekeleza mradi wa kimkakati wa kufikisha mawasiliano katika Shehia 38 zilizokua na changamoto ya mawasiliano, ambapo jumla ya minara 42 ilijengwa kwa kushirikiana na mtoa huduma Honora (YAS). Kati ya minara hiyo Mkoa wa Kaskazini Unguja ulinufaika kwa kujengewa minara 12. Mradi huu ulikamilika kikamilifu na kwasasa wananchi wananufaika na huduma za mawasiliano.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge, ameuliza swali kuhusu jitihada za Serikali katika kutatua changamoto ya mawasiliano ya simu katika vijiji vya Mkoa wa Kaskazini Unguja, inaashiria kuwa bado kuna changamoto. Wizara kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) itafanya tathmini kwenye mkoa husika ili kubaini mahitaji halisi ya mawasiliano. Endapo ikibainika kuwepo kwa tatizo la mawasiliano katika mkoa huo, utaingizwa katika zabuni ya miradi itakayotekelezwa katika Mwaka wa Fedha 2025/2026. (Makofi)
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved