Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 27 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 349 | 2025-05-19 | 
 
									Name
Godwin Emmanuel Kunambi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mlimba
Primary Question
						MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:-
Je, lini Mkandarasi atapatikana na kuanza ujenzi wa Barabara ya Morogoro hadi Njombe Border kutoka Ifakara hadi Chita?
					
 
									Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
						NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza ujenzi wa Barabara ya Ifakara – Kihansi – Mlimba – Madeke hadi Kibena yenye urefu wa kilometa 346.43 kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha, ambapo kwa sehemu ya Kwanza ya Ifakara – Mbingu (kilometa 62.5) ujenzi unaendelea na Mkandarasi wa sehemu ya Pili ya Mbingu – Chita (kilometa 37.5) ameanza maandalizi ya ujenzi.  
Mheshimiwa Spika, kwa sehemu ya Kibena – Kidegembye (kilometa 42) taratibu za ununuzi ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami zipo katika hatua za mwisho.  Aidha, kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina unaendelea kwa sehemu ya Kihansi – Mlimba hadi Madeke yenye urefu wa kilometa 95.26. Ahsante. (Makofi)
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved