Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 27 | Community Development, Gender and Children | Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum | 350 | 2025-05-19 | 
 
									Name
Bonnah Ladislaus Kamoli
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Segerea
Primary Question
						MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza:-
Je, namna gani Serikali inatekeleza takwa la Sera la ushirikishwaji wa Wazee katika shughuli za uzalishaji mali?
					
 
									Name
Mwanaidi Ali Khamis
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Sera ya Taifa ya Wazee imetambua umuhimu wa wazee kushiriki katika shughuli za kiuchumi ili kuinua kipato chao. Hivyo, Serikali kwa kushirikiana na wadau imeanzisha vikundi 395 vya uzalishaji mali vya wazee ambapo jumla ya wazee 10,926 (Me 5,333 na Ke 5,593) walinufaika na miradi mbalimbali ikiwemo ya kuwezeshwa kujihusisha na shughuli ndogo ndogo za kilimo cha mboga mboga, kuwa na vitalu vya miche ya matunda, ufugaji wa nyuki, mbuzi, ng’ombe na kuku. 
Mheshimiwa Spika, niendelee kutoa wito kwa wazee kutumia mazingira yao kufanya shughuli ndogondogo ambazo zinasaidia kuimarisha afya ya mwili na akili. Aidha, ninasisitiza jamii kuendelea kuunga mkono juhudi na shughuli zinazofanywa na wazee katika jamii zetu ili kuimarisha ustawi wao. Ahsante.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved