Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 9 | Finance and Planning | Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji | 107 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Dorothy George Kilave
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Temeke
Primary Question
						MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:-
Je, kuna mpango gani wa kutenga fedha za kujenga uzio katika Shule za Msingi na Sekondari – Temeke?
					
 
									Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa uzio kwa ajili ya ulinzi na usalama wa wanafunzi hususan maeneo ya mijini. Katika mwaka 2024/2025, Serikali ilitumia shilingi 190,735,794 kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika Shule za Msingi Wailes na Likwati na Shule za Sekondari Miburani na Nzasa zilizopo Manispaa ya Temeke.  
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2025/2026, Serikali imepanga kutumia shilingi 200,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika Shule za Msingi Kibasila, Mji mpya na Kibondemaji na Shilingi 150,000,000 katika Shule mpya za Sekondari za Chang’ombe, Makangarawe na Mwembebamia.
 
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha za ujenzi wa uzio katika shule za msingi na sekondari kupitia mapato ya ndani ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kadri ya upatikanaji wa fedha. 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved