Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 9 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 108 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Stanslaus Shing'oma Mabula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nyamagana
Primary Question
						MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-
Je, kuna mpango gani kuiongezea fedha TARURA, ili kujenga Barabara za ndani, ikiwemo ya Mkuyuni – Mahina hadi Nyakato?
					
 
									Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA, NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuiongezea bajeti TARURA kutoka shilingi bilioni 275.03 katika Mwaka wa Fedha 2020/2021 hadi shilingi bilioni 886.30 Mwaka wa Fedha 2024/2025. Barabara ya Mkuyuni – Mahina – Nyakato, yenye urefu wa kilometa 11.02 imeshafanyiwa usanifu wa kina, ambapo makadirio ya kuijenga kwa tabaka la lami ni shilingi bilioni 22. Ujenzi wa barabara hiyo kwa urefu wa kilomita mbili unatarajiwa kuanza Mwaka wa Fedha 2025/2026. (Makofi)
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved