Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 9 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 109 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Jonas Van Zeeland
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mvomero
Primary Question
						MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:-
Je, kuna mpango gani wa kujenga Daraja kuunganisha Kijiji cha Digoma na Digalama katika Mto Mjonga – Mvomero?
					
 
									Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA, NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imejenga daraja la muda la kamba za vyuma linalotumika na waenda kwa miguu pamoja na pikipiki, kwa ajili ya shughuli za usafiri na usafirishaji katika Kijiji cha Digoma na Digalama. Aidha, kazi ya usanifu wa daraja la kudumu lenye urefu wa meta 40 litakalojengwa kwa mawe imekamilika, kwa ajili ya ujenzi katika mpango wa fedha za dharura chini ya wabia Benki ya Dunia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ipo hatua za mwisho kwenye mchakato wa manunuzi, kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Daraja la Mjonga katika Barabara ya Turiani – Digoma – Digalama linalounganisha Vijiji vya Kichangani, Muhonda, Digoma na Digalama. Serikali itaendelea kuuhudumia mtandao wa barabara Wilayani Mvomero kwa kuzijenga, kuzikarabati na matengenezo, kulingana na upatikanaji wa fedha.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved