Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 9 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 111 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Amina Ali Mzee
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza:-
Je, lini suala la hedhi salama litapewa kipaumbele kwa kugawa taulo za kike bure shule za msingi na sekondari na kuboresha miundombinu ya vyoo?
					
 
									Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
						NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilishaanza kutekeleza mpango wa hedhi salama katika shule za msingi na Sekondari kwa kutoa elimu juu ya masuala ya hedhi kwa lengo la kuvunja ukimya; uwekaji wa miundombinu ya kudhibiti bidhaa za hedhi, kuhakikisha watoto wa kike wanapata bidhaa bora na salama wakati wa hedhi pamoja na utoaji wa msaada wa kijamii. Baadhi wamekuwa wakipata maumivu makali wakati wa hedhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia inatekeleza Mwongozo wa Taifa wa Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira Shuleni ambao umeweka maelekezo ya kila shule kutenga chumba kwa ajili ya kubadilishia sambamba na Mwongozo wa Usanifu wa Miundombinu ya Hedhi ambayo ni chumba cha kubadilishia ambacho kimeunganishwa na kiteketezi. Aidha, Mwongozo wa Uanzishaji na Usajili wa Shule 2020 umeweka chumba cha kujisitiri cha wasichana wakati wa hedhi kuwa miongoni mwa kigezo cha usajili wa shule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved