Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 9 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 112 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Hassan Seleman Mtenga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtwara Mjini
Primary Question
						MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaagiza mazao ya mbaazi na ufuta kusafirishwa kupitia Bandari ya Mtwara?
					
 
									Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
						NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mazao ya mbaazi na ufuta ni kati ya mazao yanayozalishwa na Mikoa ya Kusini mwa Tanzania na kuuzwa katika masoko ya Kimataifa. Tofauti na zao la korosho, usafirishwaji wa mazao hayo hufanyika, baada ya kusafishwa kwenye viwanda ambavyo vingi viko Dar es Salaam. Hivyo, usafirishaji hufanyika kupitia Bandari ya Dar es Salaam ambayo iko karibu na viwanda hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuwezesha mazao ya mbaazi na ufuta kusafirishwa kupitia Bandari ya Mtwara yakiwa na viwango vya masoko ya nje, Serikali kupitia Mamlaka ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) imetoa Tangazo (Expression of Interest) la kukaribisha kampuni zilizo tayari kujenga miundombinu ya kusafisha mbaazi na ufuta karibu na maeneo ya uzalishaji Mkoani Mtwara na Lindi. Tayari kampuni tano zimejitokeza. Baada ya mchakato kukamilika zitaunganishwa na waendesha maghala ili kuwezesha kampuni hizo kukusanya na kuhifadhi mbaazi na ufuta kabla ya kuuza kupitia minada ya kidigiti.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved