Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Hassan Seleman Mtenga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtwara Mjini
Primary Question
MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, lini Serikali itaagiza mazao ya mbaazi na ufuta kusafirishwa kupitia Bandari ya Mtwara?
Supplementary Question 1
MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali ya nyongeza mawili. 
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali tayari imeshaleta mbolea kwa ajili ya zao la korosho na kwa sasa mvua zimeshaanza kunyesha Mkoa wa Mtwara maeneo mengi ya vijijini barabara huwa hazipitiki kwa wakati. Je, ni lini Serikali itaanza sasa kugawa mbolea hizo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, msimu wa mwaka jana kulikuwa na matatizo ambayo yalijitokeza kwenye vyama vya msingi, malipo kwa wakulima wa korosho yalikuwa yanasuasua sana. Je, Serikali imejipangaje kwa mwaka huu wa msimu malipo yaende sawa bila malalamiko kwa wananchi? (Makofi)
 
											Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
								NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mheshimiwa Mtenga, kwa kufuatilia wakulima wake hususan wa zao la korosho. Jambo moja ambalo nimhakikishie tu kwamba sisi Serikali kupitia Wizara ya Kilimo tumetangaza mbolea inapofika ianze kusambazwa kwa wakulima. Nitumie forum hii kuwaambia wale mawakala wote wa usambazaji waanze kupeleka katika maeneo ambayo yamekusudiwa kuwafikia hususan katika maeneo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu malipo ya korosho, Serikali tunaendelea kuboresha utaratibu ili kuhakikisha wanalipa kwa wakati na maelekezo ambayo aliyatoa Mheshimiwa Waziri katika mwaka uliopita kwamba mkulima alipwe ndani ya siku saba na utaratibu huo umeendelea kutekelezeka. Kwa hiyo, tutaendelea kufuatilia ili kuhakikisha mkulima hacheleweshewi malipo yake. (Makofi)
							
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved