Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 9 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 113 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Angelina Adam Malembeka
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhifadhi mbegu na mimea ya asili kwa ajili ya vizazi vijavyo?
					
 
									Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
						NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali ni kuendelea kuhifadhi mbegu na mimea ya asili kwa ajili ya matumizi endelevu ya mbegu hizo. Hadi sasa, jumla ya sampuli 38,000 za mbegu na mimea ya asili zimekusanywa na kuhifadhiwa kwa ajili ya kuziendeleza. Kati ya hizo sampuli 10,000 zimehifadhiwa na Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu (TPHPA) kupitia kitengo cha Hifadhi ya Nasaba za Mimea na sampuli 28,000 zimehifadhiwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI).
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kukusanya mbegu hizo, Serikali imeanza taratibu za kujenga Benki ya Taifa ya Nasaba za Mimea (National Gene Bank) katika kituo cha TARI Selian (Arusha) ambapo kwa sasa michoro na makadirio ya ujenzi (BOQ) imekamilika kwa ajili ya kuendelea na hatua za kutangaza zabuni ya ujenzi.  Ahsante sana.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved