Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 9 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 114 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Kilumbe Shabani Ng'enda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigoma Mjini
Primary Question
						MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza:-
Je, nini mpango wa Serikali kujenga nyumba za Askari Polisi na Magereza eneo la Bangwe Kigoma Mjini?
					
 
									Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la kambi ya Polisi Bangwe lina ukubwa wa meta za mraba 25,489.8 likiwa na nyumba za makazi ya Askari Polisi 42 wanazoishi familia 88. Katika eneo hilo Serikali ina mpango wa kujenga nyumba mpya nne za ghorofa zitakazoishi familia 48, kwani nyumba zilizopo sasa ni chakavu na haziwezi kukarabatika. Eneo la kambi ya Gereza Bangwe lina ukubwa wa ekari 52 likiwa na uwezo wa kukidhi idadi ya nyumba 61 za (two in one) za kutosheleza kwa makazi ya kuishi familia 123 za askari. 
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Gereza Bangwe lina idadi ya nyumba 44 za kuishi familia 89 kukiwa na uhitaji wa nyumba 17 za kuishi familia 34. Aidha, kwa sasa Jeshi la Magereza, linaendelea na ujenzi wa nyumba mbili. Serikali kupitia Jeshi Polisi na Magereza itaendelea kutenga fedha kwenye Bajeti ya Serikali kila mwaka kwa ajili ya ujenzi wa nyumba pamoja na kuboresha makazi ya askari nchini ikiwa ni pamoja na Mkoa wa Kigoma. Ahsante. 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved