Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 1961-1995 | Session 1 | Sitting 1 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 116 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Shanif Mansoor Jamal
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwimba
Primary Question
						MHE. NG’WASI D. KAMANI K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza:-
Je, lini fedha za kuboresha mtandao wa maji kutoka Mhalo – Ngudu katika Jimbo la Kwimba zitalipwa?
					
 
									Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inafanya maboresho ya bomba la Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria kutoka Kijiji cha Mhalo kwenda Ngudu lenye umbali wa kilometa 25.4 kwa lengo la kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama. Fedha za ujenzi wa mradi huo zinatarajiwa kupelekwa mwezi Mei, 2025 ambapo utekelezaji wake unatarajiwa kufanyika kwa kipindi cha miezi 12. Uboreshaji wa mtandao wa maji kutoka Mhalo - Ngudu utakapokamilika utanufaisha wananchi wapatao 53,000 wa Mji wa Ngudu pamoja na Vijiji 16 vya Wilaya ya Kwimba vilivyopo kandokando ya bomba hilo.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved