Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 9 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 117 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Anatropia Lwehikila Theonest
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:-
Je, nini haki za Abiria wa vyombo vya moto nchini na kwa kiwango gani wanatambua haki zao?
					
 
									Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
						NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, abiria anayesafiri kwenye basi la njia ndefu (mikoani na nchi jirani), basi la mjini (daladala), teksi, pikipiki za magurudumu mawili au matatu, treni, ndege, pamoja na meli ana haki ya usalama wa chombo na mazingira salama, haki ya kuchagua chombo cha usafiri, haki ya kulipwa fidia pale anapostahili kama akipata majanga, haki ya kusikilizwa na kuelimishwa, haki ya kupewa tiketi na kufikishwa mwisho wa safari yake.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved