Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 9 | Community Development, Gender and Children | Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum | 118 | 2025-04-22 | 
 
									Name
Najma Murtaza Giga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- 
Je, Serikali ina mkakati gani wa ziada wa kulinda haki za watoto, kwani kuna ongezeko kubwa la uvunjifu wa haki za watoto nchini?
					
 
									Name
Mwanaidi Ali Khamis
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Serikali itaendelea kuweka mikakati ya ziada ya kulinda haki za watoto nchini. Aidha, mikakati hiyo ni pamoja na:-
(i)	Kutekeleza Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto wa 2024 - 2029 unaolenga kutokomeza ukatili kwa 50% ifikapo mwaka 2029;
(ii)	Kuelimisha jamii kuhusu Sheria za Ulinzi wa Mtoto, mathalani mtu anayekutwa na hatia ya kumpa mimba mwanafunzi adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 na Wazazi wasiolea na kutunza watoto adhabu ni faini isiyozidi shilingi milioni tano au kifungo miezi sita au vyote kwa pamoja
(iii)	Kuendelea kuibua Kampeni za kuelimisha Jamii kuhusu Haki za Watoto, mfano Kampeni ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia (2023 - 2025), pamoja na;
(iv)	Kuimarisha mkakati wa ulinzi na usalama wa mtoto kwenye Jamii pamoja na Madawati ya Ulinzi na Usalama wa Mtoto kwenye Shule za Msingi na Sekondari.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved