Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 484 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Esther Nicholus Matiko
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:-
Je, lini Serikali itapeleka huduma ya x-ray machine kwenye Vituo vya Afya Nkende na Kibumaye – Tarime?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI A MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa huduma za kiuchunguzi za mionzi katika vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi nchini. Katika kipindi cha mwaka 2021/2022 hadi 2024/2025 jumla ya mashine za kidijiti za x–ray 318 zimenunuliwa na kufungwa katika vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini. Aidha, Halmashauri ya Mji Tarime imepokea mashine mbili za x–ray na kuzifunga katika Hospitali ya Nyamwaga na Kituo cha Afya cha Sirare.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya kununua mashine za x–ray na kuzipeleka kwenye vituo vya afya vitakavyokuwa vimekamilisha ujenzi wa majengo ya huduma za mionzi kote nchini vikiwemo Vituo vya Afya vya Nkende na Kibumaye katika Halmashauri ya Mji wa Tarime. 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved