Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 485 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Kenneth Ernest Nollo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bahi
Primary Question
						MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: -
	
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Chifutuka – Bahi?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Chifutuka kilipokea shilingi milioni 500 mwaka 2017/2018 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la maabara, jengo la upasuaji, jengo la wazazi, chumba cha kuhifadhia maiti na nyumba ya mtumishi. Ujenzi wa majengo hayo umekamilika na majengo yanatumika. 
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya kukamilisha miundombinu inayopungua katika Kituo cha Afya cha Chifutuka.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved