Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 486 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Stella Simon Fiyao
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - 
Je, lini Serikali itaanza kujenga mifumo ya uvunaji maji ya mvua katika shule zote nchini?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, sensa ya elimu msingi ya mwaka 2024 inaonesha kuwa shule 5,311 za sekondari zina vyanzo vya maji vya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 2,960, visima ni shule 1,217 na wanaovuna maji ya mvua ni shule 1,134. Aidha,  shule 20,509 za msingi zina vyanzo vya maji vya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 10,965, visima shule 4,966 na shule zinazovuna  maji ya mvua ni 4,578.
 
Mheshimiwa Mwenyekiti, mikakati ya Serikali ya kufikisha huduma za maji safi na salama katika shule za msingi na sekondari nchini ni pamoja na ujenzi wa shule mpya au miundombinu ya vyoo kujumuisha fedha za ujenzi wa miundombinu ya kuvuna maji ya mvua.
 
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa itaendelea kuweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha shule zinakuwa na huduma ya maji safi na salama, kwa kuzingatia vyanzo vya maji vya eneo husika. 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved