Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 487 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Husna Juma Sekiboko
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -
Je, lini Serikali itakarabati mabweni ya wasichana ya kidato cha tano na sita katika Shule za Kilindi na Mlongwema?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitoa fedha za ujenzi na ukarabati wa miundombinu mbalimbali katika Shule za Wasichana Kilindi na Mlongwema kwa ajili ya kuboresha mazingara ya ujifunzaji na ufundishaji. 
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025 Serikali imetoa shilingi milioni 312 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa manne,  bweni moja, umaliziaji wa bweni moja na bwalo moja katika Shule ya Wasichana Kilindi. Aidha, bweni lililokamilishwa ni ambalo lilikuwa chakavu kutokana na  kuanza kutumika kabla ya ukamilishaji. 
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetoa shilingi milioni 578.5 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili, madarasa 11, matundu 17 ya vyoo na ukarabati wa mfumo wa maji wa bweni katika Shule ya Sekondari Mlongwema. Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati au ujenzi wa miundombinu katika maeneo mbalimbali katika shule za kidato cha tano na sita ili kuboresha mazingira ya elimu nchini. (Makofi)
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved