Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 488 | 2025-06-03 | 
 
									Name
George Natany Malima
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mpwapwa
Primary Question
						MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - 
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami unaoendelea katika Mji wa Mpwapwa?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza ujenzi wa barabara kwa tabaka la lami na uwekaji wa taa 41 katika Mji wa Mpwapwa kwa mikataba miwili yenye thamani ya shilingi bilioni 1.11 ambapo kilometa tatu zinajengwa. Mradi huo umefikia 70% na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2025.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuihudumia miundombinu ya barabara na madaraja ya Mji wa Mpwapwa kwa kuijenga, kuikarabati na kuifanyia matengenezo kulingana na upatikanaji wa fedha. (Makofi)
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved