Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 489 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Dr. Alice Karungi Kaijage
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kada nyingine wanapewa madaraja mserereko kama ilivyo kada ya ualimu?
					
 
									Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa kifungu cha 6(1)(b) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura 298 jukumu la kuwapandisha vyeo watumishi ni la mwajiri husika. Jukumu hili hutekelezwa baada ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kutoa mwongozo kuwataka waajiri kuandaa na kuwasilisha ikama na bajeti ya mwaka husika wa fedha na ofisi kuridhia utekekelezaji wa bajeti hiyo.
 
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imewapandisha vyeo kwa mserereko watumishi wasio walimu 1,284. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imetoa mwongozo unaohusu upandishaji vyeo na ubadilishaji kada ikiwemo na kwa watumishi waliocheleweshwa kupandishwa vyeo. Hivyo, nitoe wito kwa waajiri wote katika sekta ya umma kutekeleza kwa wakati mwongozo huo ili kuepusha malalamiko kwa watumishi wa umma wenye changamoto za kupandishwa vyeo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved