Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 490 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Flatei Gregory Massay
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbulu Vijijini
Primary Question
						MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -
Je, kwa nini Serikali isipeleke ajira kwenye ngazi ya halmashauri ili kuweka uwiano wa nafasi katika kila jimbo?
					
 
									Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma ya mwaka 2008, Toleo la 2 Aya ya 4.2, nafasi za ajira hutolewa kwa ushindani na kwa kuzingatia sifa stahiki kwa mujibu wa Miundo ya Maendeleo ya Utumishi ya kada husika. Vilevile mgawanyo wa nafasi za ajira mpya katika utumishi wa umma huzingatia mahitaji ya watumishi yaliyoainishwa na mwajiri na kisha kuidhinishwa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika ikama na bajeti kwa mwaka wa fedha husika. 
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Ofisi ya Rais, Utumishi kuidhinisha kibali cha ajira mpya, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma huendesha usaili wa kuwapata watahiniwa stahiki na kisha kuwapangia katika maeneo yenye uhitaji ili kujaza nafasi wazi kulingana na mahitaji ya mwajiri kwa mwaka husika. Kwa msingi huo nafasi za ajira mpya haziwezi kutolewa kwa uwiano sawa kwa kila jimbo, nashukuru.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved