Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishat | 491 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Dr. John Danielson Pallangyo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Arumeru-Mashariki
Primary Question
						MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme wa REA kwenye vitongoji 37 ambavyo vipo gizani katika Jimbo la Arumeru Mashariki? 
					
 
									Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Arumeru Mashariki lina jumla ya vitongoji 330 ambapo kati ya hivyo, vitongoji 284 vimepatiwa umeme, 17 vipo katika hatua ya utekelezaji kupitia mradi wa ujazilizi na mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji Awamu ya Pili  A. Vitongoji 29 zabuni imetangazwa ili kupata wakandarasi wa kutekeleza miradi kupitia mradi wa kupeleka umeme vitongojini Awamu ya Pili B. 
Mheshimiwa Mwenyekiti, kukamilika kwa miradi hii kutawezesha vitongoji vyote vya Jimbo la Arumeru Mashariki, kufikiwa na umeme, ahsante. (Makofi)
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved