Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 493 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Muharami Shabani Mkenge
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bagamoyo
Primary Question
						MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya umwagiliaji katika Jimbo la Bagamoyo hasa katika Mradi wa JICA?
					
 
									Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
						NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Skimu ya Bagamoyo Irrigation Development Programe (BIDP) yenye ukubwa wa hekta 100 iliendelezwa na Serikali kupitia ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) kwa lengo la kufundishia wakulima katika Kijiji cha Sanzale, Kata ya Magomeni, Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo. Skimu hiyo imeendelea kufanyiwa ukarabati na kuendelezwa na Serikali kwa awamu tofauti. 
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika mwaka wa fedha 2025/2026 imepanga kufanya maboresho ya miundombinu ya umwagiliaji katika skimu hiyo ili kuhakikisha inazalisha kwa tija na kuongeza ufanisi wa matumizi ya rasilimali maji. Kazi ya tathmini ya uchakavu wa miundombinu ya umwagiliaji kwa ajili ya kupata gharama halisi za ukarabati wa miundombinu hiyo inaendelea.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved