Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 494 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Joseph Anania Tadayo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwanga
Primary Question
						MHE. PRISCUS J. TARIMO K.n.y. MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha Miradi ya Maji Kijiji cha Mangio, Mwaniko na Msangeni – Mwanga?
					
 
									Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji Mwai-Mwaniko-Mangio uliopo Wilaya ya Mwanga, Mkoani Kilimanjaro. Kazi zinazotekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ukarabati wa matanki mawili yenye ujazo wa lita 90,000 kila moja, ujenzi wa nyumba ya mitambo (pump house), ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 17 sanjari na ujenzi wa vituo 30 vya kuchotea maji. Utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 60% na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2025 na kunufaisha wananchi wapatao 5,551 waishio kwenye Vijiji vya Mwai, Mwaniko na Mangio. (Makofi)
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved