Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Lands, Housing and Human Settlement Development | Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi | 495 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Vita Rashid Kawawa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Primary Question
						MHE. OMARI M. KIGUA K.n.y. MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: - 
Je, lini Serikali itatatua migogoro ya mipaka ya Hifadhi Kata ya Mputa na Mchomoro, Namtumbo?  
					
 
									Name
Geophrey Mizengo Pinda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
						NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI Alijibu: - 
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ina jukumu la kutafsiri Matangazo ya Serikali kuhusu Mipaka ya Hifadhi na Mipaka ya Kiutawala. Katika kutekeleza jukumu hili, Wizara yangu inashirikiana na Wizara za Kisekta, ikiwemo Wizara ya Maliasili na Utalii na Ofisi ya Rais, TAMISEMI.  
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia migogoro ya mipaka ya hifadhi katika Kata za Mputa na Mchomoro, Wilayani Namtumbo, Wizara itaunda timu ya wataalam inayojumuisha watumishi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Maliasili na Utalii na Ofisi ya Rais, TAMISEMI ambayo itashirikiana na Halmashauri za Vijiji vyenye migogoro ya mipaka katika kutatua migogoro husika. Timu hiyo inatarajia kuanza kazi kabla ya mwisho wa mwezi Juni, 2025. 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved