Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 496 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Soud Mohammed Jumah
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Donge
Primary Question
						MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - 
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka huduma za afya bure kama ilivyo katika elimu ya msingi na sekondari? 
					
 
									Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
						NAIBU WAZIRI WA AFYA Alijibu: - 
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuboresha mifumo ya ugharamiaji wa huduma za afya kwa wananchi wasio na uwezo. Tangu mwaka 1995 Serikali imekuwa ikitekeleza Sera ya Msamaha wa Gharama za Matibabu kwa Wananchi Wasio na Uwezo. Hata hivyo, kutokana na changamoto ambazo zimeendelea kujitokeza katika utekelezaji, Serikali iko katika hatua za utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote. Sheria hiyo itatoa fursa kwa watu wasio na uwezo kugharamiwa bima ya afya na Serikali ili kuwawezesha kupata huduma za afya bila kikwazo cha fedha. 
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved