Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 38 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 497 | 2025-06-03 | 
 
									Name
Condester Michael Sichalwe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Momba
Primary Question
						MHE. CONDESTER M. SICHALWE Aliuliza: - 
Je, lini Serikali itavitambua vivutio vilivyopo Jimbo la Momba kama vile Nyayo za Mtu wa Kale, Nkanyama, Maporomoko ya Mfuso na Yala (Mpona)? 
					
 
									Name
Dunstan Luka Kitandula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkinga
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII Alijibu: - 
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Wizara ilitekeleza zoezi la kutambua vivutio vya utalii katika Wilaya ya Momba kwa lengo la kuviendeleza na kuvitumia kama bidhaa za utalii. Miongoni mwa vivutio vilivyobainishwa ni Nyayo za Mtu wa Kale, Nkanyama, Maporomoko ya Mfuso na Yala (Mpona) na Kimondo cha Ivuna. Baada ya kuvibaini vivutio hivyo, zoezi linalofuata ni kufanya tathmini ya vivutio vilivyobainishwa ili kupata vivutio ambavyo viko karibu na miundombinu wezeshi kwa ajili ya kuvipa kipaumbele katika uendelezaji kwa kushirikiana na halmashauri husika na wadau wa sekta binafsi, ili kupata matokeo ya haraka. 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved