Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 30 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 380 | 2025-05-22 | 
 
									Name
Kenneth Ernest Nollo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bahi
Primary Question
						MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:-
Je, lini Serikali Itaanza Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mpalinga – Bahi?
					
 
									Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imetenga fedha ya nyongeza shilingi bilioni 53.5 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kwenye kata 214 za kimkakati. Awamu ya kwanza inaanza na ujenzi wa vituo 120 ambapo shilingi bilioni 30 zimetengwa. 
Mheshimiwa Spika, katika Halmashauri ya Bahi shilingi milioni 250 zitapelekwa awamu ya pili katika Kata ya Mtitaa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje (OPD), choo cha nje, kichomea taka na shimo la kutupia kondo la nyuma. 
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika kata za kimkakati kote nchini ikiwemo Kata ya Mpalinga katika Halmashauri ya Bahi.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved