Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 381 2025-05-22

Name

Rose Vicent Busiga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. ROSE V. BUSIGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka fedha za kukamilisha ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika Kituo cha Afya Runzewe Mashariki – Bukombe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Bukombe imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Msonga kilichopo Kata ya Runzewe Mashariki. Mpaka sasa jumla ya shilingi milioni 413.08 zimepelekwa na kutekeleza ujenzi wa jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje (OPD), jengo la maabara na jengo la kliniki ya mama, baba na mtoto (RCH). Majengo yote yamekamilika na yanatumika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe imetoa shilingi milioni 164.05 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wazazi (maternity) na jengo la upasuaji. Ujenzi wa majengo haya umefikia 85%. Aidha, katika mwaka 2025/2026 Serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri imetenga shilingi milioni 80 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la kufulia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji wa wa miundombinu ya msingi ikiwemo wodi ya mama na mtoto katika Kituo cha Afya Msonga katika Kata ya Runzewe Mashariki Ahsante.