Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 30 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 383 | 2025-05-22 | 
 
									Name
Hawa Mchafu Chakoma
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:-
Je, lini Uwanja wa Ndege Mafia utaboreshwa ili ndege kubwa ziweze kutua?
					
 
									Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
						NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa, kutokana na umuhimu wa Kiwanja cha Ndege cha Mafia katika kuhudumia watalii na wananchi kwa ujumla kiwanja hiki kina barabara nzuri ya kuruka na kutua, barabara ya kiungio na eneo la maegesho kwa kiwango cha lami. Miundombinu hiyo inawezesha ndege zenye uwezo wa kubeba takribani abiria 50 kwa wakati mmoja kama ATR 42 na fokker 50 kutumia kiwanja hiki kwa ufanisi majira yote ya mwaka (kiangazi na masika). 
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 Serikali imepanga kusimika mfumo wa taa za kuongozea ndege ili kuwezesha ndege kutua na kuruka nyakati za usiku. Mipango ya Serikali kwa miaka ya fedha ijayo ni kurefusha barabara ya kuruka na kutua pamoja na kujenga jengo jipya la abiria.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved