Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 30 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 384 | 2025-05-22 | 
 
									Name
Joseph Zacharius Kamonga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ludewa
Primary Question
						MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:-	
Je, lini Serikali itaanzisha Kituo cha Meli katika Vijiji vya Nsele na Lifuma ili kuwaondolea adha ya usafiri wananchi wa maeneo hayo?
					
 
									Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
						NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Februari 2023, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ilikamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya kuendeleleza Bandari za Mbamba Bay, Itungi, Kiwira, Ndumbi, Manda, Matema, Liuli and Lupingu. TPA ilianza utekelezaji wa ujenzi wa Bandari ya Ndumbi ambayo imekamilika. Kwa sasa TPA inaendelea na utekelezaji wa ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa Bandari zingine katika Ziwa Nyasa vikiwemo Vijiji vya Nsele na Lifuma utaendelea kufanyika kadri rasilimali fedha itakavyopatikana.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved