Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 30 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 384 2025-05-22

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanzisha Kituo cha Meli katika Vijiji vya Nsele na Lifuma ili kuwaondolea adha ya usafiri wananchi wa maeneo hayo?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Februari 2023, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ilikamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya kuendeleleza Bandari za Mbamba Bay, Itungi, Kiwira, Ndumbi, Manda, Matema, Liuli and Lupingu. TPA ilianza utekelezaji wa ujenzi wa Bandari ya Ndumbi ambayo imekamilika. Kwa sasa TPA inaendelea na utekelezaji wa ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa Bandari zingine katika Ziwa Nyasa vikiwemo Vijiji vya Nsele na Lifuma utaendelea kufanyika kadri rasilimali fedha itakavyopatikana.