Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 30 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 385 2025-05-22

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:-

Je, lini Taa za kuongozea Ndege zitafungwa katika Uwanja wa Ndege Mpanda?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunavyofahamu gharama za usimikaji na uendeshaji wa mfumo wa taa za kuongozea ndege ni kubwa na hivyo Serikali imekuwa ikitekeleza miradi hiyo katika Viwanja vya ndege vyenye miruko na mituo mingi ambayo inapelekea hitaji la mashirika ya ndege kuja nyakati za usiku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiwanja cha Ndege cha Mpanda kina miundombinu ya barabara ya kuruka na kutua ndege, barabara ya kiungio na eneo la maegesho katika kiwango cha lami na jengo jipya la kisasa la abiria na idadi ya ndege zinazotumia Kiwanja cha Ndege cha Mpanda kwa ratiba maalum ni kutoka Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) pekee ambayo inakuja na mara tatu kwa wiki Jumanne, Alhamisi na Jumamosi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, serikali inatoa wito kwa wadau mbalimbali ikiwemo mashirika ya ndege yaweze kuanzisha safari za ratiba maalum katika kiwanja hiki na Shirika la Ndege la ATCL kuongeza idadi ya miruko na mituo ili kuwezesha Serikali kusimika mfumo wa taa za kuongozea ndege.