Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 34 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 432 | 2025-05-28 | 
 
									Name
Jonas Van Zeeland
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mvomero
Primary Question
						MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: -
Je, kuna mpango gani wa kujenga shule ya sekondari Kata ya Kikeo – Mvomero?
					
 
									Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikijenga shule mpya za kata kwa ajili ya kupunguza msongamano darasani na watoto kutembea mwendo mrefu. Kupitia mpango huu Kata za Homboza, Kweuma na Mkindo za Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, tayari zimejengewa shule mpya.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2024/2025 Serikali imetenga shilingi milioni 528.99 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari ya kutwa katika Kata ya Kikeo. 
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kujenga shule za kata katika maeneo yenye shule zenye msongamano au maeneo ambayo wanafunzi wanatembea mwendo mrefu kadiri ya upatikanaji wa fedha. 
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved