Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 34 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 433 | 2025-05-28 | 
 
									Name
Eric James Shigongo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Buchosa
Primary Question
						MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: -
	
Je, Serikali inafahamu tatizo la uhaba wa walimu, hasa wa masomo ya sayansi nchini?
					
 
									Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inafahamu tatizo la uhaba wa walimu hasa masomo ya sayansi nchini. Sensa ya Elimu Msingi Mwaka 2024 inaonesha kuwa mahitaji ya Walimu wa Masomo ya Sayansi ni 31,123, waliopo ni 21,309 na upungufu ni walimu 9,814. 
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikiajiri walimu wa kada mbalimbali ikiwemo walimu wa masomo ya sayansi kadiri ya upatikanaji wa fedha. Mwaka 2024/2025 Serikali imeajiri walimu 15,925 wakiwemo walimu wa masomo ya sayansi 5,115 ambao wamepangiwa vituo vya kazi katika maeneo yenye upungufu zaidi. Serikali itaendelea kuajiri walimu wa masomo ya sayansi kadiri ya upatikanaji wa fedha.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved