Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 34 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 434 | 2025-05-28 | 
 
									Name
Asia Abdulkarim Halamga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Endagau Jimbo la Hanang?
					
 
									Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2024/2025 Serikali imetenga shilingi bilioni 53.5 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kwenye kata 214 za kimkakati, ambapo kila kituo kitapokea shilingi milioni 250. Katika Halmashauri ya Hanang, fedha hizo zitapelekwa katika Kata ya Hidet kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Endagau ina jumla ya wananchi 6,286 na iko umbali wa kilometa 8 kutoka Kituo cha karibu cha Endasak.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika kata za kimkakati na zitakazokidhi vigezo kote nchini, zikiwemo Kata za Halmashauri ya Hanang.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved