Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 34 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 435 | 2025-05-28 | 
 
									Name
Emmanuel Adamson Mwakasaka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tabora Mjini
Primary Question
						MHE. REHEMA J. MIGILLA K.n.y. MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-
Je, kuna mkakati gani wa kuondoa upungufu wa vituo vya afya katika Kata za Tabora Mjini?
					
 
									Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Manispaa ya Tabora ina jumla ya kata 29 ambapo kata tano ndio zina vituo vya afya na Hospitali ya Manispaa. Mwaka 2023/2024 Serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri imetoa shilingi milioni 275 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Itetemia ambapo ujenzi wa jengo la huduma za wagonjwa wa nje (OPD) na jengo la maabara umekamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2024/2025 Serikali imetenga shilingi milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kata ya Uyui Manispaa ya Tabora. Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika kata za kimkakati katika Manispaa ya Tabora.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved