Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 34 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 442 | 2025-05-28 |
Name
Minza Simon Mjika
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:-
Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha zao la Pamba na Alizeti linastawishwa kisasa ili kuinua uchumi wa Wananchi mkoani Simiyu?
Name
Hussein Mohamed Bashe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nzega Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali katika kuongeza tija na uzalishaji wa mazao ya kilimo ikiwemo pamba na alizeti. Mikakati hiyo ni pamoja na kusambaza mbegu za pamba tani 28,800, chupa 10,000 na vinyunyizi 100,000 vyenye thamani ya shilingi bilioni 50.11; kusambaza mbegu bora za alizeti tani 700 kwa wakulima kwa mpango wa ruzuku; kuajiri Maafisa Ugani 413 kupitia programu ya Jenga Kesho iliyo Bora kwa ajili ya kutoa huduma za ugani kwa wakulima; na kuwezesha utoaji wa huduma za ugani kwa wakulima kwa kununua na kusambaza pikipiki 179 kwa Maafisa Ugani ngazi ya kata na vijiji na gari moja ngazi ya mkoa ili kuimarisha uratibu wa ufuatiliaji wa shughuli za ugani.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali itasambaza mbegu za pamba tani 28,000, chupa 12,000,000 na vinyunyizi 100,000 kwa wakulima wa pamba pamoja na kusambaza mbegu bora za alizeti tani 2,150 kupitia mpango wa ruzuku.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved